Job 10:1-6

Ayubu: Nayachukia Maisha Yangu


1 a“Nayachukia sana haya maisha yangu;
kwa hiyo nitatoa malalamiko yangu kwa wazi bila kujizuia,
nami nitanena kutokana na uchungu wa moyo wangu.

2 bNitamwambia Mungu: Usinihukumu,
bali niambie una mashtaka gani dhidi yangu.

3 cJe, inakupendeza wewe kunionea,
kuikataa kwa dharau kazi ya mikono yako,
huku wewe ukitabasamu juu ya mipango ya waovu?

4 dJe, wewe una macho ya kimwili?
Je, wewe huona kama mwanadamu aonavyo?

5 eJe, siku zako ni kama zile za mwanadamu,
au miaka yako ni kama ile ya mtu,

6 fili kwamba utafute makosa yangu
na kuichunguza dhambi yangu;
Copyright information for SwhKC