Job 10:1-6
Ayubu: Nayachukia Maisha Yangu
1 a“Nayachukia sana haya maisha yangu;
kwa hiyo nitatoa malalamiko yangu kwa wazi bila kujizuia,
nami nitanena kutokana na uchungu wa moyo wangu.
2 bNitamwambia Mungu: Usinihukumu,
bali niambie una mashtaka gani dhidi yangu.
3 cJe, inakupendeza wewe kunionea,
kuikataa kwa dharau kazi ya mikono yako,
huku wewe ukitabasamu juu ya mipango ya waovu?
4 dJe, wewe una macho ya kimwili?
Je, wewe huona kama mwanadamu aonavyo?
5 eJe, siku zako ni kama zile za mwanadamu,
au miaka yako ni kama ile ya mtu,
6 fili kwamba utafute makosa yangu
na kuichunguza dhambi yangu;
Copyright information for
SwhKC